Skip to main content

mashambulio

Katika picha hii ya maktaba, wanakijiji kutoka  Ogossagou,  jimbo la  Mopti  nchini Mali baada ya shambulio la tarehe 23 Machi mwaka 2019 na kusababisha vifo vya watu 160 na wengine 70 walijeruhiwa, mamia kupoteza makazi.
UNICEF/Maiga

Watu 95 wauawa nchini Mali, MINUSMA yalaani vikali

Mashambulizi dhidi ya raia wasio na hatia Mali ni ukatili usiostahili na unaopaswa kushughulikiwa haraka, umesema leo mpango wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini humo MINUSMA baada ya shambulio la jana jioni kukatili maisha ya raia wengi kwenye Kijiji cha Sobanou-Kou kilichopo Kaskazini Mashariki mwa mji wa Bandiagara, kwenye jimbo la Mopti.