Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen, hii leo akihutubia Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kwa njia ya video kutoka Amman,Jordan ameonya kuwa mgawanyiko nchini Yemen umekuwa wenye nguvu zaidi na wa kutisha zaidi kuliko awali.