Maria Ressa

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akizungumza na waandishi wa habari mjini New York Marekani
UN News

Hakuna jamii itakayokuwa huru na haki bila waandishi wa Habari:Guterres 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza waandishi wa Habari Maria Ressa na Demirty Muratov kwa kushinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu akisema “Duniani kote uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu kwa ajili ya amani, haki, maendeleo endelevu na haki za binadamu na ni ngumo muhimu kwa ajili ya ujenzi wa taasisi zenye haki na zisizo na upendeleo.” 

08 OKTOBA 2021

Katika jarida la mada kwa kina hii leo Assumpta Massoi anakuletea

-Waandishi wa habari Maria Ressa raia wa Ufilipino na Dimitry Muratov raia wa Urusi wameshinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu 2021

-Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la mpango wa chakula duniani WFP, la elimu sayansi na utamaduni UNESCO na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wamewapongeza na kuwamwagia sifa washindi hao kwa mchango wao katika kusongeza njia ya amani

Sauti
21'4"
Picha kutoka kwenye video wakati Maria Ressa alipokuwa akishiriki mkutano wa UNESCO kuhusu uhuru wa vyombio vya habari. (Mei 4, 2020)
UNESCO

UNESCO leo imekabidhi tuzo ya Guillermo Cano kwa Maria Ressa

Mwandishi wa habari wa uchunguzi wa Ufilipino leo ametunukiwa tuzo  ya heshima kwenye hafla iliyoandaliwa iliyoandaliwa na Serikali ya Namibia na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO katika mji mkuu Windhoek, nchini Namibia ambako wataalamu wa vyombo vya habari wanataka hatua za dharura zichukuliwe dhidi ya vitisho na kudhoofishwa kwa uhuru wa habari kote ulimwenguni.