Hakuna jamii itakayokuwa huru na haki bila waandishi wa Habari:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewapongeza waandishi wa Habari Maria Ressa na Demirty Muratov kwa kushinda tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu akisema “Duniani kote uhuru wa vyombo vya habari ni muhimu kwa ajili ya amani, haki, maendeleo endelevu na haki za binadamu na ni ngumo muhimu kwa ajili ya ujenzi wa taasisi zenye haki na zisizo na upendeleo.”