Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Maria Fernanda Espinosa

Picha kutoka juu ya mji wa Bogotá, Colombia.
World Bank/Dominic Chavez

Umoja wa Mataifa walaani vikali tukio la kigaidi mjini Bogota Colombia.

Katiku Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulio la bomu katika chuo cha polisi mjini Bogota nchini Colombia. Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake Stéphane Dujarric jijini New York, Marekani, Guterres ametuma pia salamu zake za rambirambi kwa familia za waathirika wa shambulio hilo la jana Alhamisi na akawatakia ahueni ya haraka wote waliojeruhiwa katika tukio hilo la bomu lililotegwa katika gari na kusababisha vifo vya takribani watu 21 na makumi walijeruhiwa.