Miaka miwili ya vita Gaza wananchi bado wanateseka
Kwa miongo kadhaa, Israel na Palestina zimekuwa katika migogoro ya mara kwa mara. Lakini tarehe 7 Oktoba mwaka 2023, hali ilibadilika ghafla.
Kwa miongo kadhaa, Israel na Palestina zimekuwa katika migogoro ya mara kwa mara. Lakini tarehe 7 Oktoba mwaka 2023, hali ilibadilika ghafla.
Hatma ya bidhaa nyingi za kilimo na viwandani kutoka Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kuelekea Marekani ipo mashakani kufuatia kumalizika kwa muda wa Mpango wa Ukuaji na Fursa za Afrika (AGOA), hatua ambayo inaweza kudhoofisha juhudi za nchi za bara hilo kupanua mauzo yao ya nje ya malighafi limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo, UNCTAD.
Rais wa Marekani – Donald J. Trump akihutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 80 hii leo jijini New York amejinasibu kwamba amefanikiwa kumaliza mogogoro siyokwisha “Katika kipindi cha miezi saba, nimemaliza vita saba ambavyo havikuisha “amedai Rais huyo.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo lilipewa taarifa na afisa mkuu wa masuala ya siasa wa Umoja wa Mataifa kuhusu shambulio la anga la Israel mjini Doha Qatar na kusema ni ongezeko la kutisha la mvutano lililolaaniwa kama uvunjaji wa mamlaka ya nchi unaotishia mazungumzo yanayoendelea ya kusitisha mapigano na kuachiliwa kwa mateka huko Gaza.
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, amelaani vikwazo vipya vilivyowekwa na Marekani dhidi ya majaji na manaibu waendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Makao ya Jinai ICC, akisema hatua hiyo inahatarisha misingi ya utawala wa sheria.
Hii leo jaridani tunaangazia mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, na juhudi za kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro Sudan Kusini. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya.
Baada ya mashambulizi ya ghafla ya anga yaliyofanywa na Marekani dhidi ya vituo vya kurutubisha urani vya Iran mwishoni mwa wiki, mkuu wa shirika la kimataifa la nishati ya Atomiki IAEA, linaloungwa mkono na Umoja wa Mataifa, leo limetoa wito wa kuruhusiwa mara moja kufika kwenye maeneo hayo ili kutathmini kiwango cha uharibifu ambacho huenda kikawa kikubwa zaidi.
Baraza la Usaama la Umoja wa Mataifa leo limekutana kwa dharura mjini New York Marekani kujadili hatari ya amani na usalama wa kimataifa kufuatia mashambulizi ya jana yanayodaiwa kufanywa na Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA), Rafael Mariano Grossi, ametangaza kwamba ataitisha kikao cha dharura cha Bodi ya Magavana ya shirika hilo kufuatia kuzorota kwa hali ya usalama wa nyuklia nchini Iran baada ya mashambulizi dhidi ya vituo muhimu vya nyuklia yaliyofanywa jana Jumamosi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa onyo kali usiku huu wa Jumamosi kufuatia taarifa ya matumizi ya nguvu ya Marekani dhidi ya Iran, akilitaja tukio hilo kuwa “uchochezi hatari na tishio la moja kwa moja kwa amani na usalama wa kimataifa.”