Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo amelaani vikali mashambulio yote katika maeneo yaliyo na watu wengi ndani na katika viunga bvya ukanda wa mapigano wa Nagorno-Karabakh, wakati duru zikiripoti kwamba pande zote katika mgogoro huo za Azerbaijan na Armenia zikilaumiana kwa kukiuka makubaliano ya karibuni ya usitishaji uhasama kwa misingi ya kibinadamu.