Bila udhibiti mzuri wa hatari ya majanga, hali mbaya huzidi kuwa mbaya zaidi-Guterres
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kupunguza hatari ya majanga, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametahadharisha kuwa janga la COVID-19 limeleta umakini mpya kuhusu umuhimu wa kuimarisha upunguzaji wa hatari za majanga kwani hali mbaya zinazidi kuwa mbaya zaidi pindi panapokosekana udhibiti mzuri wa hatari za majanga.