Tumuenzi Malkia Elizabeth kwa kufanya kazi kwa bidii ili tuwe UN ya kweli- Katibu Mkuu
Jua limezama kwa mtawala wa aina yake! Ndivyo alivyoanza hotuba yake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo kwenye ukumbi wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, ambamo wawakilishi wa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa walikutana katika tukio maalum la kuenzi Malkia Elizabeth wa II wa Uingereza aliyega dunia tarehe 8 mwezi huu wa Septemba huko Scotland.