Skip to main content

Malkia Elizabeth II

Mwaka 2010, Malkia wa Elizabeth wa II wa Uingereza akiweka shada la maua kwenye eneo la kukumbuka watumishi wa UN waliopoteza maisha yao wakihudumia shirika.
UN /Evan Schneider

Tumuenzi Malkia Elizabeth kwa kufanya kazi kwa bidii ili tuwe UN ya kweli- Katibu Mkuu

Jua limezama kwa mtawala wa aina yake! Ndivyo alivyoanza hotuba yake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo kwenye ukumbi wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, ambamo wawakilishi wa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa walikutana katika tukio maalum la kuenzi Malkia Elizabeth wa II wa Uingereza aliyega dunia tarehe 8 mwezi huu wa Septemba huko Scotland.

12 SEPTEMBA 2022

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza kwa taarifa ya kwamba utumwa wa kisasa una aina mbalimbali ikiwemo kwenye ajira na pia kwenye ndoa. Kisha anakupeleka kaunti ya Tukrana nchini Kenya ambako UNICEF imenusuru wanawake na mwendo mrefu wa kusaka maji kwa kuwajengea mabwawa ya mchanga. Makala anakukutanisha na Hamad Rashid wa redio washirika MVIWATA FM mkoani Morogoro akikuletea mradi wa UNCDF ambao umekwamua maisha ya wakazi wa Kibondo mkoani Kigoma Tanzania kupitia ushirika wa kilimo uitwao Kibondo Big Power Group.

Sauti
11'48"