Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Malakal

©UNMISS Video

Muziki waunganisha jamii zilizogawanyika Malakal nchini Sudan Kusini

Katika juhudi za kuimarisha mshikamano na kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, hivi karibuni waliandaa tamasha maalum la muziki katika mji wa Malakal, jimbo la Upper Nile – eneo ambalo kwa miezi ya hivi karibuni limekuwa kitovu cha machafuko. Sharon Jebichii anatupasha zaidi

Sauti
2'5"

23 JUNI 2025

Hii leo jaridani tunaangazia mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, na juhudi za kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro Sudan Kusini.  Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya.

Sauti
10'27"
Msanii maarufu wa Sudan Kusini Emmanuel Kembe, ambaye alitumbuiza wakazi Malakal Sudan Kusini kwa nyimbo zenye ujumbe wa amani na mshikamano.
©UNIMISS Video

Muziki waunganisha jamii zilizogawanyika Malakal, Sudan Kusini

Katika juhudi za kuimarisha mshikamano na kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, hivi karibuni waliandaa tamasha maalum la muziki katika mji wa Malakal, jimbo la Upper Nile – eneo ambalo kwa miezi ya hivi karibuni limekuwa kitovu cha machafuko.

Sauti
2'5"
IOM/Bannon

Sitisha uhasama miongoni mwa wakimbizi wa ndani Sudan Kusini: UNMISS 

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umetoa wito wa kusitishwa mara moja kwa uhasama miongoni mwa wakimbizi wa ndani katika Kambi ya Umoja wa Mataifa ya Ulinzi wa Raia nchini humo kufuatia tukio la jana Alhamis ambapo watu kadhaa waliripotiwa kujeruhiwa na wengine kuuawa.

Video iliyorekodiwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) inaonesha gari la wagonjwa la Umoja wa Mataifa likisindikizwa na walinda amani likipita katika barabara ya vumbi katikati ya umati wa wakimbizi wa ndani katika eneo la Malakal nchini Sudan Kusini.  

Sauti
2'22"
UN Photo/Isaac Gideon

Malakal Sudan Kusini watumia bendi ya muziki inayoeneza amani

Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS, wanashirikiana na washirika wake wa amani, watu wa Sudan Kusini, kuleta sauti zinazotetea amani ya kudumu katika nchi mpya zaidi ulimwenguni lakini inayoendelea kuteseka na migogoro, vifo na kutawanywa, miaka kadhaa tangu vita ya wenyewe kwa wenyewe. John Kibego na maelezo zaidi.

Ni watoto wa Sudan Kusini wakiwa wameshikilia gitaa kila mmoja, wamekalia viti vya kamba, kila mmoja amevaa barakoa wanafuata kwa umakini maelekezo ya mwalimu wao wa muziki. 

Sauti
2'14"