Palestina yasema iko njiapanda, yamtaka Guterres aitishe kongamano la kimataifa la amani
Rais wa Taifa la Palestina Mahmoud Abbas ametoa wito kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuitisha mkutano wa kimataifa kuhusu amani na ili kuhakikisha kuwa mpango huo hauna mkwamo Israel lazima iondoke kutoka Ukingo wa Magharibi wa mto Jordan, Ukanda wa Gaza na Yerusalem Mashariki katika kipindi cha mwaka mmoja.