Dola bilioni 1.7 zahitajika kusaidia wananchi wa Sudan Kusini
Mzozo nchini Sudan Kusini ukiingia mwaka wa nne, zaidi ya dola bilioni 1.7 zahitajika ili kukidhi mahitaji ya kibinadamu kwa nchini humo kwa mwaka 2018.
Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu nchini humo Alain Noudéhou ametangaza kiwango hicho hii leo kwenye mji mkuu, Juba akisema mpango huo unalenga watu milioni 6 walioathiriwa zaidi na mzozo, kupoteza makazi, njaa na kudorora kwa uchumi.