Wataalamu wa UN wajiunga kutetea wananchi wa Zambia walioathiriwa na uchimbaji madini
Mahakama nchini Afrika Kusini imewaruhusu wataalamu wa Umoja wa Mataifa kushiriki kwenye kesi iliyofunguliwa na wananchi wa wilaya ya Kabwe nchini Zambia walioathirika na madini ya risasi kwenye uchimbaji wa madini uliofanywa na Kampuni ya madini ya Anglo American.