Mabwawa ya mchanga

12 SEPTEMBA 2022

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza kwa taarifa ya kwamba utumwa wa kisasa una aina mbalimbali ikiwemo kwenye ajira na pia kwenye ndoa. Kisha anakupeleka kaunti ya Tukrana nchini Kenya ambako UNICEF imenusuru wanawake na mwendo mrefu wa kusaka maji kwa kuwajengea mabwawa ya mchanga. Makala anakukutanisha na Hamad Rashid wa redio washirika MVIWATA FM mkoani Morogoro akikuletea mradi wa UNCDF ambao umekwamua maisha ya wakazi wa Kibondo mkoani Kigoma Tanzania kupitia ushirika wa kilimo uitwao Kibondo Big Power Group.

Sauti
11'48"