Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya tabianchi 

Wahudumu wa afya wakifanya operesheni ya kunyunyizia dawa ya kutokomeza mbu aina ya Anopheles. Mbu huyu ndiye aenezaye ugonjwa wa Malaria.
WHO

Dengue na Chikungunya yatia hofu, Zika kuna unafuu – WHO

Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO limetoa mwelekeo wa magonjwa ya Dengue, Chikungunya na Zika duniani, ambapo kwa Dengue idadi kubwa ya wagonjwa imeripotiwa Sudan, huku hofu ikiongezeka kutokana na kuenea kwa Chikungunya katika nchi za Amerika ya Kusini ilhali kwa Zika kuna nuru kwani idadi ya wagonjwa imepungua.