Mjadala wa wazi wa ngazi ya mawaziri kuhusu mabadiliko ya tabianchi na usalama, viongozi watoa maoni
Viongozi wa ngazi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa hii leo wametumia mjadala wa wazi wa ngazi ya mawaziri kuhusu tabianchi na usalama uliofanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, kutoa maoni yao na wasiwasi walionao kuhusu mabadiliko ya tabianchi.