Wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameihimiza serikali ya Nicaragua ikomeshe ukandamizaji kufuatia siku 100 za maandamano ambapo watu takriban 317 wameuawa ilhali wengine 1,830 wamejeruhiwa.
Wahudumu wa afya huko Gaza, Mashariki ya Kati hivi sasa wanahaha kutibu zaidi ya majeruhi 2700 wa ghasia za jana zilizosababisha vifo vya watu 58. Taarifa zaidi an Assumpta Massoi.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema imepokea taarifa za kuaminika kwamba takriban watu 25 wameuawa nchini Nicaragua wakati wa maandamno ya nchi nzima dhidi ya mipango ya kufanyia mabadiliko mfumo wa hifadhi ya jamii.
Mratibu maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati, Nickolay Mladenov, amesema anafuatilia kwa hofu kubwa maandalizi ya maandamano makubwa ya marejeo yaliyopangwa kufanyika Kesho Ijumaa Ukanda wa Gaza.
Chondechonde Iran shughulikieni kwa uangalifu wimbi la maandamano yanayoendelea nchin humo, amesema Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Zeid Ra’ad Al Hussein katika taarifa yake aliyotoa hii leo.
Umoja wa Mataifa umesema unafuatilia kwa karibu hali inayoendelea nchini Iran ambako maandamano yanayodaiwa kuwa ni ya kupinga serikali yameingia siku ya tano huku watu 22 wakiripotiwa kuuawa.