Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu, OHCHR hii leo imetoa taarifa yake ikipazia sauti mwenendo wa maandamano yanayoendelea maeneo mbalimbali dunia ikisema kuwa ni kiashiria tosha cha wananchi kuchoshwa au kuchukizwa na serikali zao hususan kutokana na hali ngumu za kiuchumi na kijamii, ufisadi, ukosefu wa usawa na kuongezeka kwa pengo la walio nacho na wasio nacho.