Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema anafuatilia kwa karibu hali inayoendelea hivi sasa nchini Uganda na kusema anatiwa hofu na ripoti za machafuko na mauaji kufuatia maandamano yanayofanyika mjini Kampala.
Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq na mkuu wa mpango wa Umoja huo UNAMI amesema kuendelea kupotea kwa Maisha ya vijana na umwagaji damu wa kila siku ni hali ambayo haiwezi kuvumilika nchini humo.