Ripoti ya maendeleo ya binadamu iliyozinduliwa leo na Umoja wa Mataifa inasema suala la kuchukulia kila hali kuwa mazoea haliwezi kutatua changamoto za kizazi hiki kilichoghubikwa na pengo la usawa.
Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet amesema ana wasiwasi mkubwa juu ya ghasia zinazoendela nchini Sudan ambazo hadi sasa zimesababisha kuuawa kwa watu 24 na wengine wengi wamejeruhiwa.