Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Lugha ya mama

20 FEBRUARI 2023

Hii leo jaridani linaangazia lugha ya mama tunapoelekea katika siku ya Lugha ya Mama Duniani, na huduma za afya nchini Syria baada ya tetemeko la ardhi.  Makala tutakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Uganda.

Sauti
11'4"
UNESCO

Watoto wa jamii za kiasili na wale wa jamii za wachache wafundishwe kwa lugha yao wenyewe - mtaalam wa UN

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya makabila madogo, kupitia ripoti yake aliyoiwasilisha hii leo mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi amesema ni lazima watoto wanaotoka  jamii za wachache, wafundishwe kwa lugha yao inapowezekana ili kufikia lengo la ujumuishwaji na elimu bora pamoja na kuheshimu haki za binadamu za watoto wote.

Sauti
2'3"
IOM/A. Deng 2018

Lugha ya kityaba iko hatarini kupotea nchini Uganda

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya lugha ya mama hii leo Umoja wa Mataifa umesema lugha na utofauti wake wa utambulisho, kuwasiliana, kushirikiana kijamii, elimu na maendeleo ni muhimu kwa ajili ya binadamu na sayari dunia. Hatahivyo kukua kwa utandawazi kumesababisha lugha nyingi kuwa hatarini kupotea na iwapo lugha inapotea basi utofauti wa utamaduni unapotea na hivyo kuathiri kiungo muhimu cha jamii hizo. Nchini Uganda lugha ya kityaba inakabiliwa na hatari hii ambapo jamii wenyeji wa lugha hiyo wanahofu kubwa na lugha yao, kulikoni? Ungana na John Kibego katika Makala ifuatayo.

Sauti
3'45"

Lugha ya mama ni muaroabaini wa kufanikisha SDGs- UNESCO

Kila wiki mbili zinapopita, lugha moja ya asili inayotumika duniani inatoweka! Amesema Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoaj wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay katika ujumbe wake wa siku ya lugha ya mama duniani hii leo.

Hawa ni wamasai katika moja ya burudani zao kupitia lugha yao ya mama! UNESCO inasema  kuwa lugha ya mama ni msingi wa kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, kwani matumizi ya lugha ya mama yanawezesha mtu kupokea maarifa mapya kwa urahisi kuliko kupitia lugha ya mapokeo au lugha ya kigeni.

Sauti
1'39"