Lugha mama ni silaha na urithi wetu lazima kuidumisha: Wakaazi Kenya
Lugha na utamaduni vina muingiliano katika maisha ya kila siku. Hii ni kwa sababu vyote ni vipengele muhimu vya kujieleza katika jamii.
Lugha na utamaduni vina muingiliano katika maisha ya kila siku. Hii ni kwa sababu vyote ni vipengele muhimu vya kujieleza katika jamii.
Hii leo jaridani linaangazia lugha ya mama tunapoelekea katika siku ya Lugha ya Mama Duniani, na huduma za afya nchini Syria baada ya tetemeko la ardhi. Makala tutakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Uganda.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya lugha ya mama, shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO limehimiza watu kila mahali kukumbatia utofauti uliopo duniani kwa kuunga mkono lugha mbalimbali mashuleni na katika maisha ya kila siku.
Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya makabila madogo, kupitia ripoti yake aliyoiwasilisha hii leo mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi amesema ni lazima watoto wanaotoka jamii za wachache, wafundishwe kwa lugha yao inapowezekana ili kufikia lengo la ujumuishwaji na elimu bora pamoja na kuheshimu haki za binadamu za watoto wote.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya lugha mama, Umoja wa Mataifa umepigia chepuo lugha ya Kiswahili ikisema kuwa ni miongoni mwa lugha inayozidi kupanuka kimatumizi duniani na kusaidia kueneza utamaduni wake. Anold Kayanda na ripoti kamili.
Wakati dunia ikiadhimisha siku ya lugha ya mama hii leo Umoja wa Mataifa umesema lugha na utofauti wake wa utambulisho, kuwasiliana, kushirikiana kijamii, elimu na maendeleo ni muhimu kwa ajili ya binadamu na sayari dunia. Hatahivyo kukua kwa utandawazi kumesababisha lugha nyingi kuwa hatarini kupotea na iwapo lugha inapotea basi utofauti wa utamaduni unapotea na hivyo kuathiri kiungo muhimu cha jamii hizo. Nchini Uganda lugha ya kityaba inakabiliwa na hatari hii ambapo jamii wenyeji wa lugha hiyo wanahofu kubwa na lugha yao, kulikoni? Ungana na John Kibego katika Makala ifuatayo.
Leo ni siku ya lugha ya mama duniani ambapo Umoja wa Mataifa unapigia chepuo matumizi ya lugha ya mama katika mifumo yote ya maisha iwe elimu, biashara kwa lengo la kuimarisha amani, ustawi na utangamano miongoni mwa watu wenye makabila, lugha na tamaduni tofauti.
Leo ni siku ya lugha ya mama duniani ambapo Umoja wa Mataifa unapigia chepuo matumizi ya lugha ya mama katika mifumo yote ya maisha iwe elimu, biashara kwa lengo la kuimarisha amani, ustawi na utangamano miongoni mwa watu wenye makabila, lugha na tamaduni tofauti.
Lugha ya mama inasalia ndio msingi wa kumwezesha binadamu kujikwamua na maisha yake. Umfundishapo kwa kutumia lugha ya mapokeo atatumia muda mrefu kuelewa lakini ukitumia lugha ya mama uelewa ni wa haraka zaidi na una tija.
Kila wiki mbili zinapopita, lugha moja ya asili inayotumika duniani inatoweka! Amesema Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoaj wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay katika ujumbe wake wa siku ya lugha ya mama duniani hii leo.
Hawa ni wamasai katika moja ya burudani zao kupitia lugha yao ya mama! UNESCO inasema kuwa lugha ya mama ni msingi wa kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, kwani matumizi ya lugha ya mama yanawezesha mtu kupokea maarifa mapya kwa urahisi kuliko kupitia lugha ya mapokeo au lugha ya kigeni.