Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

lugha

Photo: UNESCO/M. Ravassard

Siku ya Kiswahili duniani ni Julai 7: UN

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO leo limeitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Leah Mushi na taarifa zaidi

Taarifa hiyo imetangazwa leo kwenye makao makuu ya UNESCO mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wan chi wanachama wa shirika hilo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa twitter wa UNESCO azimio maalum la kuitangaza siku hiyo limepitishwa na wanachama wote bila kupungwa.

Sauti
53"
UN

Neno la wiki-BIRUKUA

Katika kujifunza Kiswahili , leo tunapata ufafanuzi wa neno "BIRUKUA" na mchambuzi wetu ni   Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili  la Taifa  nchini Tanzania , BAKITA 

Sauti
54"
UNESCO

Watoto wa jamii za kiasili na wale wa jamii za wachache wafundishwe kwa lugha yao wenyewe - mtaalam wa UN

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya makabila madogo, kupitia ripoti yake aliyoiwasilisha hii leo mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi amesema ni lazima watoto wanaotoka  jamii za wachache, wafundishwe kwa lugha yao inapowezekana ili kufikia lengo la ujumuishwaji na elimu bora pamoja na kuheshimu haki za binadamu za watoto wote.

Sauti
2'3"
Lugha mbalimbali
UNESCO

Mataifa lazima yafundishe watoto wa kiasili na wale wa jamii za wachache kwa lugha yao wenyewe - mtaalam wa UN

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya makabila madogo, kupitia ripoti yake aliyoiwasilisha hii leo mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi amesema ni lazima watoto wanaotoka  jamii za wachache, wafundishwe kwa lugha yao inapowezekana ili kufikia lengo la ujumuishwaji na elimu bora pamoja na kuheshimu haki za binadamu za watoto wote.

Sauti
2'3"
UN News Kiswahili

Neno la Wiki-Matumizi ya neno AFADHALI.

Aida Mutenyo, mwenyekiti wa idara za Kiswahili katika vyuo vikuu Afrika Mashariki anachambua matumizi ya neno TAFADHALI.  Anasema kuwa nchini Uganda neno hili ni moja ya maneno yanayowasumbua wazungumzaji wa kiswahili kwani wanalichanganya na neno AFADHALI.

Sauti
1'48"
UN News/Assumpta Massoi

Kazi yetu ni muhimu lakini mara nyingi haijulikani- Mfasiri

Tafsiri kutoka lugha moja  hadi nyingine imekuwa ina mchango mkubwa katika utekelezaji wa majukumu ya Umoja wa Mataifa, amesema Lydie Mpambara, mmoja wa wafasiri wa lugha kwenye idara ya Baraza Kuu na mikutano  ya Umoja huo, DGACM.

Akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ikiwa sehemu ya maadhimisho ya siku ya tafsiri ya lugha duniani iliyoadhimishwa hivi karibuni, Bi. Mpambara ambaye anazungumza kiingereza, kifaransa, Kiswahili na kispanyola amefafanua jinsi kazi yao inavyochagiza majukumu ya Umoja wa Mataifa.

Sauti
2'23"