Siku ya Kiswahili duniani ni Julai 7: UN
Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO leo limeitangaza rasmi tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.
Leah Mushi na taarifa zaidi
Taarifa hiyo imetangazwa leo kwenye makao makuu ya UNESCO mjini Paris Ufaransa wakati wa mkutano wan chi wanachama wa shirika hilo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa twitter wa UNESCO azimio maalum la kuitangaza siku hiyo limepitishwa na wanachama wote bila kupungwa.