Utapiamlo umeongezeka kwa asilimia 25 kwenye nchi zenye migogoro na kuweweka wanawake na watoto hatarini: UNICEF
Wakati nusu ya watoto wote wa chini ya umri wa miaka 2 waliodumaa wakati wa ujaizito au wa chini ya umri wa miezi sita wako katika nchi zenye mizozo ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF iliyotolewa leo inasisitiza haja ya kuwekeza katika program za lishe kwa wasichana vigori na wanawake.