Skip to main content

Chuja:

lishe

Agnes Juma na watoto wake wawili, yeye ni mama wa watoto watano kutoka Kilifi Kenya,  ambaye ni mnufaika wa mradi wa NICHE.
UNICEF Kenya

Mradi wa NICHE wa afya na malezi umekua mkombozi kwa familia Kilifi Kenya: UNICEF

Kaunti ya Kilifi iliyoko Pwani ya Kenya ni moja ya maeneo ambako mradi wa majaribio wa elimu ya malezi na lishe kwa watoto unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF unafanyika kwa ushirikiano na serikali na wadau wengine, lengo kubwa likiwa ni kuzisaidia familia zisizojiweza na zilizo hatarini kupitia program ya lishe na elimu ya afya  ziweze kutoa malezi bora kwa watoto wao huku zikikabiliana na ukatili katika familia hasa dhidi ya watoto.

Sauti
4'13"
Lishe maalum inayotolewa na WFP imeboresha hatua kwa hatua utapiamlo mkubwa nchini Sudan, na familia pia zimepokea chakula kama vile unga, maharagwe makavu, mafuta na chumvi.
© WFP/Mohammed Awadh

Mapigano Sudan yanaweza kuwatumbukiza mamilioni kwenye njaa: WFP

Mlipuko wa ghasia nchini Sudan una uwezekano wa kuwatumbukiza mamilioni zaidi ya watu kwenye njaa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limelazimika kusimamisha kwa muda shughuli za kutoa msaada wa chakula na pesa zinazookoa maisha katika nchi ambayo theluthi moja ya watu tayari wanatatizika kupata chakula cha kutosha imeeleza taarifa iliyotolewa leo mjini Roma-Italia na Khartoum-Sudan.

Msichana akinywa maji katika  bustani wa shule yake huko Goré, kusini mwa Chad.
© UNICEF/Frank Dejongh

UNESCO: Mafanikio ya elimu yanatatizwa na ukosefu wa uwekezaji katika afya na lishe

Wakati kuwekeza katika afya na lishe shuleni kuna athari chanya kwa ufaulu wa watoto kitaaluma, shule 1 kati ya 3 duniani bado haina maji ya kunywa na vifaa vya msingi vya usafi wa mazingira, kulingana na ripoti mpya iliyozinduliwa leo 8 Februari na mashirika ya Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO, la kuhudumia watoto UNICEF, na la mpango wa chakula duniani WFP.

© UNICEF/James Ekwam

Kiwanda cha tiba lishe ni mkombozi kwa watoto wenye unyafuzi Pembe ya Afrika

Nchini Kenya, mfululizo wa misimu mitano bila mvua umeathiri maisha ya jamii zilizo hatarini. Vyanzo vya maji vimekuwa mbali, mimea imekauka, mifugo nayo imekufa. Mambo yote haya yamesababisha watu kutokuwa na uhakika wa kupata chakula, halikadhalika kupungua kwa uzalishaji wa maziwa, bei za vyakula zimepanda, bei za nishati huku uwezo wa watu kununua bidhaa umeporomoka.

Sauti
4'58"
© UNICEF/Yves Nijimbere

Huduma ya RapidPro iliyoletwa na UNICEF imeokoa watoto wetu Turkana nchini Kenya – Wazazi

Kaunti ya Turkana nchini Kenya inakabiliwa na ukame wa muda mrefu. Ili kusaidia kuimarisha mifumo ya lishe, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, nchini Kenya limeanzisha mfumo wa simu za mkononi uitwao RapidPro. Huduma hii huwezesha vituo vya afya kushirikishana ujumbe wa lishe na wafanyakazi wa kujitolea wa afya ya jamii, ambao huripoti taarifa na takwimu mbalimbali za kiafya kuhusu jamii zao. 

Sauti
3'45"