Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao kujadili wapiganaji mamluki wanaojiunga na vikundi vya kigaidi, jambo ambalo linatishia amani na usalama duniani.
Akihutubia kikao hicho, mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili ugaidi Vladimir Voronkov amesema suala la wapiganaji mamluki kutumikia vikundi vya kigaidi ni jambo gumu na linalobadilika kila uchao.
Amewapatia wajumbe takwimu zinazoonyesha makadirio kwamba wapiganaji zaidi ya elfu 40 kutoka zaidi ya mataifa 110 wamejiunga na vikundi vya kigaidi vinavyopigana huko Syria na Iraq.