Skip to main content

Chuja:

leah mushi

Wapiganaji mamluki wanaelekea Libya na Yemen- Voronkov

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na kikao kujadili wapiganaji mamluki wanaojiunga na vikundi vya kigaidi, jambo ambalo linatishia amani na usalama duniani.

Akihutubia kikao hicho, mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili ugaidi Vladimir Voronkov amesema suala la wapiganaji mamluki kutumikia vikundi vya kigaidi ni jambo gumu na linalobadilika kila uchao.

Amewapatia wajumbe takwimu zinazoonyesha makadirio kwamba wapiganaji zaidi ya elfu 40 kutoka zaidi ya mataifa 110 wamejiunga na vikundi vya kigaidi vinavyopigana huko Syria na Iraq.

WHO yahaha kukabili mlipuko wa dondakoo Yemen

Shirika la afya ulimwenguni, WHO limeanza kusambaza dawa ili kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa dondakoo nchini Yemen.

Mwakilishi wa WHO nchini Yemen Dkt, Nevio Zagaria amesema hatua hiyo ni muhimu ili kuondoa aibu itokanayo na watoto kufariki dunia kwa ugonjwa huo wenye chanjo.

Amesema tayari shehena ya dawa za kutibu ugonjwa huo imewasili baada ya njia za anga, majini na ardhini kufunguliwa kufuatia kufungwa kwa wiki tatu.