Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo ametoa wito wa kuwepo na juhudi za kina kupambana na uharamia kwenye pwani ya Somalia, akisema hali hiyo ni matokeo ya ukosefu wa usalama, kutokuwepo na serikali imara na umasikini kwenye taifa hilo la pembe ya Afrika.