Pata muhtasari wa kile kitakachokuwemo katika wavu wetu mpya utakaozinduliwa rasmi tarehe 01 Februari mwaka huu wa 2018. Halikadhalika fahamu sababu za kuleta wavuti huu mpya. Wenyeji wako ni Flora Nducha na Siraj Kalyango.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema kusambaratisha waandamanaji si njia sahihi ya kumaliza mzozo, badala yake inachochea zaidi. John Kibego na maelezo zaidi.,
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mauaji ya waandamanaji huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisema kitendo hicho hakikubaliki.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC watu sita wameuawa jumapili kwenye mji mkuu Kinshasa wakati wa maandamano yaliyoandaliwa na kanisa katoliki nchini humo. John Kibego na ripoti kamili.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeelezea simanzi na masikitiko yake kufuatia vifo vya wakimbizi 13 wa Syria karibu na mpaka wa Masnaa Mashariki mwa Lebanon. Kwa mujibu wa shirika hilo wakimbizi hao waliganda kwa theluji kali hadi kufa wakijaribu kuingia nchini Lebanon usiku kukiwa na baridi ya kupindukia kupiti njia ya usfirishaji haramu.