Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

KJP

UN News

Asante FAO kwani sasa nimeweza kujipatia zaidi ya dola Elfu 3 kupitia kilimo cha kisasa

Wanawake wa vijijini wanatambuliwa kimataifa kupitia siku yao ya kimataifa inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 15 mwezi Oktoba. Mwaka huu maadhimisho yamefanyika maeneo mbalimbali duniani ikiwemo mkoani Kigoma, magharibi mwa Tanzania, huko Afrika Mashariki. Shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na chakula, FAO liliandaa tukio maalum la kutambua mchango wa wanawake hao hasa kwa kuzingatia mchango wao katika uzalishaji chakula, kwani shirika la Umoja wa Mataifa la kazi, ILO linasema wanawake ni zaidi  ya asilimia 40 ya nguvukazi kwenye sekta ya kilimo.

Sauti
4'45"

18 OKTOBA 2022

Hii leo jaridani Assumpta Massoi anakuletea Mada Kwa Kina kuhusu harakati za Umoja wa Mataifa za kutokomeza umaskini kwenye mkoa wa Kigoma nchini Tanzania kupitia mashrika yake yanayotekeleza Mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP lakini pia kuna Habari kwa Ufupi zikimulika:

Sauti
11'43"
UNCDF

Ufadhili wa UNCDF umetukwamua sana Kibondo Big Power Group

 

Kibondo Big Power Group (KBPG) ni ushirika wa kilimo mkoani Kigoma, kaskazini magharibi mwa Tanzania. Shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa, UNCDF lilisaidia KBPG kwa msaada wa kifedha ambao ulitumika kupanua shughuli zake kwa kufanya shughuli zifuatazo: kuchimba kisima cha maji mita 100, ununuzi wa pampu ya maji ya jua na ujenzi wa ghala na nyumba za kukausha jua za mihogo na chanja na mtaji wa kufanyia kazi. Hamad Rashid wa redio washirika  Hamad Rashid wa redio washirika wa Redio washirika wetu MVIWATA FM ya mkoani Morogoro, Tanzania anasimulia zaidi.

Sauti
3'52"

19 AGOSTI 2022

Hii leo jaridani tunamulika siku ya kimataifa ya usaidizi wa binadamu duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anatoa shukrani kwa wale wote wanaojitolea kuchukua hatua kusaidia wengine hata wenyewe wakiwa bado na shida, huku akikumbuka wale waliopoteza maisha wakisaidia wengine. Tunakwenda pia Mexico huko ambako taka za mwani zinatengeneza matofali. Makala tunabisha hodi Kigoma, Leah Mushi anakuletea simulizi ya wanawake wanufaika wa miradi inayotekelezwa na UNDP chini ya KJP. Mashinani ni wito kutoka kwa Mkuu wa WHO ili kusaidia wakazi wa jimbo la Tigray nchini Ethiopia.

Sauti
11'48"
UN News/Assumpta Massoi

Asante UNDP Tanzania sasa wanawake Kigoma tunaona matunda ya kuweko kwenye vikundi

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP limejizatiti kusaidia mipango ya kuinua wanawake na vijana kwa  kupatia makundi hayo mitaji. Hilo linafanyika mkoani Kigoma nchini Tanzania ambako uweko wa wakimbizi ulibainika kuleta changamoto katika upatikanaji wa  mahitaji siyo tu kwa wakimbizi bali pia kwa jamii za wenyeji ambao wanawapatia hifadhi.

Sauti
4'46"