Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

kivu kusini

UN News/Byobe Malenga

Redio Ngoma ya Amani inachangia utunzaji wa amani hapa mashariki mwa DRC - Wasikilizaji

Katika Siku ya Redio Duniani mwaka huu wa 2023, UNESCO inaangazia redio huru kama nguzo ya kujenga amani na kuzuia migogoro. 

Redio inatazamwa kama chombo muhimu na sehemu muhimu ya kutunza amani. Redio hushughulikia visababishi na vichochezi vya migogoro, kabla hazijaweza kulipuka na kuwa vurugu. Inatoa mbinu mbadala ya kuzuia migogoro, au migongano ya maslahi, kuondoa kutoelewana, na kutambua masuala ya kutoaminiana. Hii inaweza kusaidia kukabiliana na chuki, hamu ya kulipiza kisasi, au nia ya kutumia silaha. 

Sauti
4'25"
Wakimbizi kutoka Burundi wakichota maji katika kambi ya Lusenda, Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo, DRC.
UNHCR/Colin Delfosse

Mlinda Amani wa Umoja wa Mataifa auwawa nchini DRC

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulio lililotokea hapo jana tarehe 30 Septemba 2022 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC katika kambi ya COB iliyopo chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO na kusababisha kifo cha mlinda amani mmoja raia wa Pakistan.

© UNICEF/Patrick Brown

Watoto watumikishwao DRC wapaza sauti zao

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 wanatumikishwa kwenye kazi mbalimbali ikiwemo uchimbaji madini, ujenzi wa nyuma, na hata sokoni kwa lengo la kukidhi mahitaji ya familia za kutokana na hali ya umaskini. Mashirika ya kutetea hali ya watoto yanachukua hatua kusihi serikali kuhakikisha sheria za kumlinda mtoto zinazingatiwa ikiwemo kwenye machimbo ya madini. Lakini hali iko vipi , mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa huko DRC, Byobe Malenga amevinjari kwenye mji wa Bukavu jimboni Kivu Kusini ili kujionea hali halisi.
Sauti
3'20"

19 Aprili 2022

Karibu jaridani hii leo na Grace Kaneiya akianzia Uganda ambako UNICEF na serikali ya Iceland wamefanikisha  mradi wa kuhakikisha huduma ya maji safi na kujisafi (WASH) kwa wanafunzi wote kwenye shule za wilaya za Adjumani na Arua nchini Uganda. Kisha anabisha hodi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC huko serikali imepatia wakimbizi na wenyeji ardhi ya ekari 500 kuimarisha kujitegemea, mkimbizi katoa shukrani. Jarida linasalia huko huko DRC kumulika juhudi za UNICEF kuona watoto wanasoma licha ya kuishi kwenye vituo vya ukimbizini.

Sauti
12'51"
Akarurimana James ni mkimbizi kutoka Burundi ambaye amenufaika na ardhi iliyotolewa na serikali ya DRC kwa ajili ya wakimbizi na wenyeji wao kwa lengo la kuimarisha kujitegemea.
UN/Byobe Malenga

Wakimbizi wa Burundi nchini DRC washukuru kupatiwa ardhi ya kilimo

Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, serikali imetangaza kutenga ekari  500 za ardhi kwa ajili ya kilimo itakayotumiwa na wakimbizi kutoka Burundi pamoja na wenyeji, kwa lengo la kuimarisha hali ya kujitegemea na kuishi pamoja kwa amani. Kwa kiasi kikubwa wakimbizi hao wamekuwa wakitegemea msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na jamii za wenyeji zinazowahifadhi wakimbizi hao.  

Sauti
2'12"