Hali ya usalama mashariki mwa DRC bado si shwari- UN
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limejulishwa kuwa hali ya usalama huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC inazidi kuwa mbayá wakati huu ambapo vikundi vya waasi vinashamirisha mashambulizi dhidi ya raia katika majimbo ya Ituri, Kivu Kaskazini na Kivu Kusini.