Zaidi ya watu laki 7 walioathiriwa na Kimbunga Gombe, Msumbiji bado wanahitaji usaidizi - IOM
Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) lina wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa mahitaji ya kibinadamu ya watu zaidi ya 700,000 walioathirika katika Mkoa wa Nampula nchini Msumbiji, kufuatia kimbunga cha Gombe ngazi ya 3 ambacho kilianguka kwenye pwani kati ya wilaya za Mossuril na Mogincual tarehe 11 Machi.