Kufuatia hali mbaya iliyosababishwa na kimbunga Dorian kaskazini mwa visiwa vya Bahama, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anaendelea kuwa na wasiwasi kuhusu maelfu ya watu walioathirika katika kisiwa cha Grand Bahama na Abaco, imeeleza taarifa yake aliyoitoa hii leo jumatano kupitia kwa msemaji wake.