Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Kimbunga

Familia ya raia wa Burundi mbele ya nyumba yao iliyoharibiwa na kimbunga Gombe, katika makazi ya wakimbizi ya Maratane, Msumbiji.
© UNHCR/Juliana Ghazi

Kimbunga Gombe, Msumbiji, UNHCR na wadau wanaharakisha msaada kwa maelfu

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR pamoja na serikali ya Msumbiji na washirika wa kibinadamu, wanaharakisha kusaidia maelfu ya familia zilizoathiriwa na kimbunga cha Tropiki cha Gombe, ambacho kilipiga katika jimbo la Nampula mnamo tarehe 11 ya mwezi huu wa Machi na kuharibu nyumba, maji kufunika mashamba, na kuwalazimisha watu kuyakimbia makazi yao ili kutafuta usalama.   

Nchini Madagaska, Rachelle Elien, afisa wa masuala ya kibinadamu wa OCHA na mwanachama wa timu ya dharura ya UNDAC, hukutana na watu walioathirika baada ya Kimbunga cha Emnati.
Chris Monnon / Atlas Logistique / OCHA

Kimbunga Emnati kuongeza zahma Madagascar:WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP limesema kimbunga Emnati kilichoikumba Madagascar Jumatano ya wiki hii (23/02/2022) kikiwa kimbunga cha nne kulikumba taifa hilo katika wiki kadhaa kinatishia uhakika wa chakula na ni mfano wa kjinsi gani cangamoto za mabadiliko ya tabianchi zisiposhughulikiwa zinaweza kusababisha mahitaji makubwa ya kibinadamu. 

© WFP/Sandaeric Nirinarison

Umoja wa Mataifa waendelea kutoa misaada ya dharura Madagascar

Kwa kipindi cha mwezi mmoja tu, nchi ya Madagascar imekabiliana na vimbunga vinne. Jumanne iliyopita, kimbunga Emnati kiliathiri maeno yaleyale yaliyoathirika na kimbunga Batsirai na kuwafurusha makwao maelfu ya watu. Umoja wa Mataifa unashirikiana na wadau wa kibinadamu na serikali ya Madagascar kuwasaidia wale wanaohitaji misaada ya dharura.

Sauti
2'13"