Kimbunga Gombe, Msumbiji, UNHCR na wadau wanaharakisha msaada kwa maelfu
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR pamoja na serikali ya Msumbiji na washirika wa kibinadamu, wanaharakisha kusaidia maelfu ya familia zilizoathiriwa na kimbunga cha Tropiki cha Gombe, ambacho kilipiga katika jimbo la Nampula mnamo tarehe 11 ya mwezi huu wa Machi na kuharibu nyumba, maji kufunika mashamba, na kuwalazimisha watu kuyakimbia makazi yao ili kutafuta usalama.