Skip to main content

Chuja:

kigoma

17 APRILI 2023

Hii leo jaridani tunasalia hapa makao makuu kukuletea yaliyojiri kwenye Jukwaa la kudumu la watu wa asili, na pia kukupeleka nchini DRC kumulika faida ya mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga. Makala tunaangazia SDG 17 na Mashinani tunakupeleka nchini Tanzania, kulikoni?

Sauti
12'55"
UNICEF

Hakikisho la maji safi na salama lachochea jamii kuishi na utangamano Mkoani Kigoma nchini Tanzania

Ufumbuzi wa ubunifu wa maji unaotumia teknolojia ya nishati ya jua ambao unafanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na wadau wake ukiwemo ule wa utekelezaji, Water Mission, na ule wa kutoa msaada wa fedha Grundfos Foundation kutoka nchini Denmark umesaidia serikali ya Tanzania kubuni suluhisho la msingi na la kudumu la maji katika jamii 15 za mkoa wa Kigoma ulioko magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki. Lengo lao kubwa ni kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa watu 99,107 mkoani humo ifikapo Machi 2024. 

Sauti
5'48"

18 OKTOBA 2022

Hii leo jaridani Assumpta Massoi anakuletea Mada Kwa Kina kuhusu harakati za Umoja wa Mataifa za kutokomeza umaskini kwenye mkoa wa Kigoma nchini Tanzania kupitia mashrika yake yanayotekeleza Mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP lakini pia kuna Habari kwa Ufupi zikimulika:

Sauti
11'43"
UNCDF

UNCDF wamenipatia elimu na kuniunganisha na taasisi za kifedha – Mkurugenzi Nabuhima Foods  

Aaron Mwimo kwa jina la utani Joti, ni mmoja wa watu wanaochangia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa, SDGs kwa kuleta ustawi bora kwa jamii yake wilayani Kibondo, mkoa wa Kigoma nchini Tanzania.  

Bwana Mwimo alianzisha kiwanda kidogo cha kuchakata mazao ya wakulima kama vile mahindi na mihogo na akakipa kiwanda chake kidogo jina Nabuhima Food Supplies akisambaza unga katika mji eneo dogo la mji wa Kibondo hadi pale alipounganishwa na shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa.  

Sauti
4'58"
UNCDF

Ufadhili wa UNCDF umetukwamua sana Kibondo Big Power Group

 

Kibondo Big Power Group (KBPG) ni ushirika wa kilimo mkoani Kigoma, kaskazini magharibi mwa Tanzania. Shirika la mitaji la Umoja wa Mataifa, UNCDF lilisaidia KBPG kwa msaada wa kifedha ambao ulitumika kupanua shughuli zake kwa kufanya shughuli zifuatazo: kuchimba kisima cha maji mita 100, ununuzi wa pampu ya maji ya jua na ujenzi wa ghala na nyumba za kukausha jua za mihogo na chanja na mtaji wa kufanyia kazi. Hamad Rashid wa redio washirika  Hamad Rashid wa redio washirika wa Redio washirika wetu MVIWATA FM ya mkoani Morogoro, Tanzania anasimulia zaidi.

Sauti
3'52"

12 SEPTEMBA 2022

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanza kwa taarifa ya kwamba utumwa wa kisasa una aina mbalimbali ikiwemo kwenye ajira na pia kwenye ndoa. Kisha anakupeleka kaunti ya Tukrana nchini Kenya ambako UNICEF imenusuru wanawake na mwendo mrefu wa kusaka maji kwa kuwajengea mabwawa ya mchanga. Makala anakukutanisha na Hamad Rashid wa redio washirika MVIWATA FM mkoani Morogoro akikuletea mradi wa UNCDF ambao umekwamua maisha ya wakazi wa Kibondo mkoani Kigoma Tanzania kupitia ushirika wa kilimo uitwao Kibondo Big Power Group.

Sauti
11'48"
UNHCR/Georgina Goodwin

Wakimbizi wa Burundi wapewa vyeti vya kuzaliwa Tanzania

Asante Tanzania mwanangu sasa atajulikana alipozaliwa :Mkimbizi Evangeline 
Familia za wakimbizi wa Burundi wanaoishi kwenye kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma nchini Tanzania wameishuru serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki kwa kuwapatia nyaraka muhimu za watoto wao, vyeti vya kuzaliwa wakati wa ziara ya Kamisha Mkuu wa wakimbizi Filippo Grandi iliyokamilika mwishoni mwa wiki. Happiness PPalangyo na taarifa zaidi

Sauti
2'1"

29 AGOSTI 2022

Flora Nducha anakuletea jarida lililo sheheni habari mbalimbali kuanzia nchini Ethiopia ambapo tume ya Kimataifa ya wataalamu wa Haki za binadamu nchini Ethiopia imekasirishwa na kuzuka upya kwa uhasama kati ya serikali ya Ethiopia na chama cha Tigray People's Liberation Front tangu wiki iliyopita na kuzitaka pande zote mbili kurudi kwenye meza ya mazungumzo kwani wanaoteseka ni raia.

Wakimbizi wa Burundi wakioko katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma nchini Tanzania wameshukuru kwa watoto wao kupatiwa vyeti vya kuzaliwa 

Sauti
10'26"