Mradi wa FISH4ACP unaotekelezwa na shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO kwa ubia na Muungano wa Afrika na ule wan chi za Karibea na Pasifiki, kwa ufadhili kutoka Muungano wa Ulaya na serikali ya Ujerumani, umeleta matumaini na mafanikio kwa wavuvi wa ziwa Tanganyika mkoani Kigoma nchini Tanzania kufuatia mafunzo waliyopatiwa wavuvi hao.