Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Kibera

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi ya wasichana ya Shofco, Kibera nchini Kenya wakizungumza na mwalimu wao.
UN News/Thelma Mwadzaya

Elimu ya mtoto wa kike ni moja ya nguzo muhimu katika jamii

Elimu ya mtoto wa kike ni moja ya nguzo muhimu katika jamii ukizingatia malengo endelevu ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa.Wakati ulimwengu unaadhimisha miaka 30 tangu Azimio la Beijing na Jukwaa la Hatua za Utekelezaji kuwekwa bayana, serikali zimetangaza nia ya kisiasa ya kuheshimu, kudumisha haki, usawa na wanawake na wasichana kuwezeshwa.

© UN-Habitat /Julius Mwelu

Tunaandaa mashindano mbalimbali ya michezo ili kuwaondoa vijana kwenye mawazo mabaya - ETCO

Mara kwa mara Umoja wa Mataifa umeendelea kusisitiza kuwa vipaji vikiwemo vya michezo vina mchango mkubwa katika kusaidia kuleta maendeleo na amani.

Vijana wanapotambuliwa vipawa vyao wanapata shughuli rasmi za kufanya na hivyo kuinua vipato vyao, kuwaondoa katika mazingira hatarishi na faida nyingine za ujumla ambazo muunganiko wake unasaidia kuelekea katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Sauti
3'7"
© Julius Mwelu/ UN-Habitat

Michezo na vipaji vingine, mkombozi wa vijana, Kibera Kenya

Umoja wa Mataifa unaamini kuwa michezo inaweza kusaidia kuchukua jukumu katika kujenga mnepo na katika kupona dhidi ya janga la COVID-19. Vile vile Umoja wa mataifa unaamini kuwa michezo ina mchango mkubwa katika kuleta maendeleo na amani. Nchini Kenya, katika mtaa wa mabanda, Kibera jijini Nairobi, wakfu wa UWEZA unajaribu kuwasaidia vijana kuweza kujitegemea kwa kutumia vipaji vyao. Miongoni mwa vipaji vinavyolengwa ni pamoja na uchezaji wa mpira wa miguu na uchoraji.

Sauti
4'17"
UN-Habitat/Nathan Kihara

Tunahifadhi mazingira huku tukijipatia kipato-Vijana Kibera, Kenya.

Kutokana na ukosefu wa ajira kwenye nchini  nyingi  ni kawaida watu kutafuta na kubuni njia za kukidhi mahitaji  yao ya kila siku. Mtaani Kibera mjini Nairobi, vijana wameanzisha kikundi ambacho hivi sasa  kinaendelea na mradi ya kukusanya taka na kuzitumia kuunda vifaa mbalimbali kisha kuviuza kupitia mradi ujulikanao kama 'Slum going green and clean', ikiwa pia ni njia ya kusafisha mazingira. Jason Nyakundi amezungumza na kiongozi wa kikundi hicho Brian Nyabut

Sauti
3'21"

22 JULAI 2020

Katika Jarida la Habari za UN hii leo Flora Nducha anakuletea 

-Mkimbizi kutoka Afghanistan aliyepatiwa hifadhi katika kijiji kimoja nchini Ufaransa sasa alipa fadhilia kwa kutumia talanta yake ya ufundi cherahani, anashona barako na kuzigawa bure kwa jamii inayomuhifadhi

-Mafunzo ya ujasiriliamali yanayotolewa na mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD kwa kushirikiana na serikali ya Norway na Niger yaleta nuru kwa vijana wakimbizi mjini Diffa Niger

Sauti
11'44"

22 APRILI 2020

Leo katika jarida la Umoja wa Mataifa Flora Nducha anakuletea

-Umoja wa Mataifa unasema janga la virusi vya Corona au COVID-19 ni kengele ya kuiamsha dunia kuchukua hatua kulinda sayari hiyo na watu wake  hasa leo ikiadhimishwa siku ya kimataifa ya mama sayari dunia

- Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na jiji la Nairobi wanachukua hatua kudhibiti kusambaa wa virusi vya corona au COVID-19, kwenye makazi dunia ya Kibera.

Sauti
12'44"
UN-Habitat/Nathan Kihara

Wanaoishi katika makazi duni wanahitaji mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:UN-HABITAT

Mamilioni ya watu wanaoishi katika mitaa ya mabanda au makazi dunia kote duniani wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo miundombinu mibovu, ukosefu wa maji safi na salama n ahata hali mbaya ya Maisha lakini kubwa zaidi kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la makazi duniani UN-HABITAT ni kutokuwa na mnepo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Shirika hilo linasema vimbunga au mafuriko yanapozuka wao huwa wa kwanza kuathirika na hasara yake ni kubwa Zaidi kuliko wengine.

Sauti
4'8"