Elimu ya mtoto wa kike ni moja ya nguzo muhimu katika jamii
Elimu ya mtoto wa kike ni moja ya nguzo muhimu katika jamii ukizingatia malengo endelevu ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa.Wakati ulimwengu unaadhimisha miaka 30 tangu Azimio la Beijing na Jukwaa la Hatua za Utekelezaji kuwekwa bayana, serikali zimetangaza nia ya kisiasa ya kuheshimu, kudumisha haki, usawa na wanawake na wasichana kuwezeshwa.