Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

katibu mkuu umoja wa mataifa

UM ‘waibana koo’ Myanmar

Serikali ya Myanmar imepewa miezi sita kuwasilisha kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ripoti maalumu ya hali ya wanawake na wasichana wa kabila la Rohingya kutoka jimbo la kaskazini la Rakhine.

Uamuzi huo umetolewa na kamati ya mkataba wa kimataifa wa kutokomeza ubaguzi wa aina zote dhidi ya wanawake, CEDAW huko Geneva, Uswisi, kama yenye jopo la wataalamu 23 wa Umoja wa Mataifa.