Chuja:

katibu Mkuu

24 JANUARI 2023

Ni Jumanne ya tarehe 24 mwezi Januari mwaka 2023 ambapo leo tunakwenda nchini Tanzania kuangalia juhudi zinavyofanyika kuhakikisha wanafunzi hususan wa vijijini wanakuwa na mazingira bora ya kuweza kujisomea  nyakati zote. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikimulika hali ya usalama DR Congo, ujumbe wa Katibu Mkuu ya siku hii ya elimu duniani na ripoti ya usafirishaji haramu wa binadamu. Katika mashinani tunakupeleka nchini Kenya.

Sauti
13'7"
UNICEF/Zayat

Vita dhidi ya ISIL vyaingia awamu mpya- Voronkov

 

Vita dhidi ya kikundi cha wapiganaji wa ISIL au Da’esh bado ni changamoto duniani na vinahitaji hatua za dharura na za pamoja.

Hayo yemetamkwa na mkuu wa ofisi ya Umoja wa mataifa inayohusika na kukabiliana na ugaidi Vladimir Voronkov wakati akihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani kuhusu hali ya ugaidi hususan wa kundi hilo la ISIL kwa sasa.

Bwana Voronkov alikuwa akigusia ripoti ya Katibu Mkuu kuhusu ISIL ambapo wametaka juhudi za pamoja  katika kufanikisha juhudi zao.

(Sauti ya Vladmir Voronko)

Sauti
1'58"

Idadi ya majeruhi DRC sasa ni 63, Guterres apaza sauti

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mauaji ya waandamanaji huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akisema kitendo hicho hakikubaliki.

Yaelezwa kuwa wakati wa maandamano hayo watu 6 waliuawa ilihali idadi ya majeruhi sasa ni 63.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric akizungumza na waandishi wa habari mjini New  York, Marekani hii leo amesema..

(Sauti ya Stephane Dujarric)