Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Karamoja

06 NOVEMBA 2023

Hii leo jaridani Assumpta Massoi anaanzia Mashariki ya Kati, mapigano huko Gaza siku ya 30, "imetosha" yasema mashirika ya kimataifa, kisha anakwenda Gambia, Magharibi mwa Afrika huko kalavati limeimarisha afya. Makala ni kijana Emmanuel Cosmas Msoka akizungumza na Flora Nducha kuhusu SDGs na mashinani tunakwenda Karamoja nchini Uganda, kilimo cha kisasa kimekomboa wanawake kiuchumi na kijamii. 

Sauti
12'59"
WFP

UNICEF: Kila msichana anastahili fursa nyingine ya elimu hata kama alijifungua akiwa shuleni

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na serikali ya Uganda kupitia msaada wa serikali ya Ireland, unawapa fursa ya pili ya kurejea shuleni wasicha waliopata ujauzito na waliojifungua kabla ya kumaliza masono katika jimbo la Karamoja nchini Uganda. Lengo kuu la mradi huo ni kuhakikisha hakuna msichana yeyote anayesalia nyuma kielimu hata kama amekuwa mama katika umri mdogo.

Sauti
3'3"
Nanjala Suzan ni mama kijana mwenye umri wa miaka 15. Yeye ni mmoja wa wasichana vijana waliosajiliwa katika Shule ya Msingi Katwe kunufaika na mpango wa Hifadhi ya Jamii unaolenga wasichana wadogo wa shule katika Wilaya ya Kampala Uganda.
© UNICEF

Kila msichana anastahili fursa nyingine ya elimu hata kama alijifungua akiwa shuleni: UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na serikali ya Uganda kupitia msaada wa serikali ya Ireland, unawapa fursa ya pili ya kurejea shuleni wasichana waliopata ujauzito na waliojifungua kabla ya kumaliza masomo katika jimbo la Karamoja nchini Uganda. Lengo kuu la mradi huo ni kuhakikisha hakuna msichana yeyote anayesalia nyuma kielimu hata kama amekuwa mama katika umri mdogo.

Sauti
3'3"
Picha: WHO Video screenshot

WHO na wadau waingilia kati kupambana na utapiamlo mkali unaosababishwa na athari za ukame Pembe ya Afrika

Ukame katika ukanda wa Pembe ya Afrika umeleta madhara makubwa kwa ustawi wanadamu na ikolojia nzima katika eneo hilo. Madhara ya moja kwa moja yaliyoshuhudiwa na watu wa ukanda huo zikiwemo nchi za Somalia, Kenya, Ethiopia na maeneo ya kaskazini mwa Uganda ni ukosefu wa chakula na hivyo kusababisha utapiamlo hasa utapiamlo mkali kwa watoto.

Mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la Afya Ulimwenguni, WHO na wadau wake, wameingilia kati ili kupunguza makali ya tatizo hilo kama si kulimaliza kabisa. Anold Kayanda ameangazia hatua hizo na kutuandalia makala ifuatayo.

Sauti
3'3"

28 DESEMBA 2022

Hii leo jaridani tunakuletea habazi za UNCTAD na kazi za Umoja wa Mataifa nchini CAR. Makala tunakupeleka Karamoja nchini Uganda na mashinani tunakuletea ujumbe wa WFP kuhusu mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
9'58"