06 NOVEMBA 2023
Hii leo jaridani Assumpta Massoi anaanzia Mashariki ya Kati, mapigano huko Gaza siku ya 30, "imetosha" yasema mashirika ya kimataifa, kisha anakwenda Gambia, Magharibi mwa Afrika huko kalavati limeimarisha afya. Makala ni kijana Emmanuel Cosmas Msoka akizungumza na Flora Nducha kuhusu SDGs na mashinani tunakwenda Karamoja nchini Uganda, kilimo cha kisasa kimekomboa wanawake kiuchumi na kijamii.