Eh Mungu geuzia uso wako kwa wana Sudan Kusini- Mkimbizi
Tangu mwezi disemba mwaka 2013, Sudan K usini imekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Maelfu ya watu wamekimbilia nchi jirani na wengine wamesaka hifadhi kwenye maeneo mengine ya nchi. Hata hivyo hivi sasa wengine wameamua kurejea na kilio chao sasa ni kwa mwenyezi Mungu.