Skip to main content

Chuja:

Kabul

© WFP

Ndege za misaada zaruhusiwa kutua uwanja wa ndege wa Kabul

Ndege za shirika la Anga la Umoja wa Mataifa zinazosimamiwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP zimeanza tena safari zake za kupeleka msaada Kabul nchini Afghanistan na kuwawezesha wafanyakazi wa kibinadamu kuwafikia wananchi wenye uhitaji. 

(Taarifa ya Leah Mushi)

Nchini Afghanistan zaidi ya asilimia 90 ya wananchi wanahaha kupata mlo wa familia, Ghulam Dastagir mwenye umri wa miaka 58, baba wa familia ya watu 10 anasema maisha ni magumu mno.

Sauti
2'34"

Jarida 15 Septemba 2021

Katika jarida hii leo utasikia jukwaa maalum lililoanzishwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO kwa ajili ya elimu ya kung'atwa na nyoka. Nchini Senegal mradi wa kunusuru mikoko umesaidia wavuvi kuongeza kipato na nchini Afghanistan ndege za misaada zaanza kushusha chakula na vifaa vya matibabu. 

Ungana na Assumpta Massoi kwa undani wa taarifa hizo.

Sauti
14'27"
Mtoto akitembea katika kambi ya muda ya Kabul baada ya familia yake kuyakimbia makazi yao kutokana na mzozo nchini Afghanistan
© UNICEF Afghanistan

Shambulio la kigaidi Kabul ni msumari wa moto juu ya kidonda kwa Waafghanistan:UN

Ofisi ya Kamisnina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa imesema shambulio la kigaidi lililofanywa na kundi la ISIL-Khorasan kwenye uwanja wa Ndege wa Kabul nchini Afghanistan jana ni ililikuwa hatua na uamuazi mbaya wa kundi hilo, nani bayana lilikuwa limepangwa kuua na kulemaza watu wengi iwezekanavyo wakiwemo raia, watoto, wanawake, kina baba, kina mama, pamoja na Taliban na vikosi vya kigeni vinavyolinda uwanja wa ndege.

UNAMA/Eric Kanalstein

Mradi wa Mfereji wa Maji waboresha maisha ya wakazi wa Kabul, Afghanistan

Kila siku wananchi watano katika kijiji cha Pazhaki jimboni Kabul nchini Afghanisan walikuwa wanajukumu la kufungulia maji katika mfereji uliokuwa unategemewa na wanakijiji hao kwa shughuli za kilimo. Lakini Ramazan Ibrahimkil, mwenyekiti wa Kijiji cha Pazhak anasema alikuwa anapokea kesi kila uchwao kwamba wananchi wanaokaa milimani wakilalamikiwa kufungulia maji kwa wingi na hivyo wale wa mabondeni kukosa maji ya kutosha kwenye kilimo chao na hivyo kupata mazao machache na kipato kidogo. 

Sauti
4'41"