Wanawake nchini Afghanistan wameendelea kubeba mzigo zaidi wa madhara yatokanayo na mzozo uliodumu nchini humo takribani miongo minne sasa, amesema Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed wakati akihutubia Baraza la Usalama la umoja huo hii leo jijini New York, Marekani.