Chuja:

jukwaa la vijana

UN Video

Vijana tunachagiza mabadiliko ya kisera ili kulinda bahari - Nancy Iraba

Mkutano wa pili wa kimataifa kuhusu bahari unaendelea huko Lisbon, Ureno. Mkutano huu umeanza tarehe 27 mwezi huu wa Juni na utamalizika tarehe 1 Julai 2022. Kabla ya kuanza kwa kikao cha ngazi ya juu, mkutano ulitanguliwa na jukwaa la vijana likileta pamoja wanaharakati na wachechemuzi vijana kuhusu masuala ya baharí wakionesha ubunifu wao wa jinsi ya kutatua dharura ya baharí, kama alivyooiita Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres .Miongoni mwa washiriki ni kijana Nancy Iraba mwanasayansi wa masuala ya bahari kutoka Chuo Kikuu cha Dare es salaam nchini Tanzania. Hapa akihoijwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa anaelezea jukwaa linajikita na nini.

Sauti
1'32"
Rais wa ECOSOC, Inga Rhonda King (Katikati) akihutubia jukwaa la vijana la baraza hilo la uchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa.
UN / Evan Schneider

Vijana tunyanyuane hii itatusaidia zaidi- Jayathma

Jukwaa la vijana la Baraza la Uchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa, ECOSOC, limeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani likileta pamoja wawakilishi zaidi ya 1000 wa vijana kutoka kona mbalimbali pamoja na mawaziri wa vijana kutoka nchi wanachama wa umoja huo kuzungumzia harakati za kunasua vijana na kile kinachofanyika mashinani kuchagiza mchango wa vijana katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.