Skip to main content

Chuja:

Jubaland

Ahmad Hassan Yarow mwenye umri wa miaka 70 katika kambi ya wakimbizi wa ndani Luuq nchini Somalia
UN Photo/Fardosa Hussein

Katika umri wangu wa miaka 70 sijashuhudia ukame wa kiwango hiki- Mwananchi Somalia

Akiwa amesimama mbele ya kibanda chake kwenye makazi ya wakimbizi ya Kulmiye wilayani Luuq nchini Somalia, Ahmad Hassan Yarrow anatazama kile kilichosalia katika mto Juba, ambao ulikuwa ndio tegemeo la uhai wa  eneo lao. Mto umekauka. “Katika umri wangu wa miaka 70 sijawahi kushuhudia ukame kama huu, katika vipindi vyote vya ukame vilivyopita,” anasema Bwana Yarrow katika makala iliyochapishwa kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa usaidizi nchini Somalia, UNSOM.

Sauti
3'4"
Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, James Swan akihutubia Baraza la Usalama.
UN Photo/Manuel Elías

Usalama wa Somalia bado ni wa wasiwasi, aonya Mkuu wa UNSOM

Katika hotuba yake ya kwanza kwa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani hii leo, mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, James Swan ameeleza hatua ilizozipiga Somalia katika kuboresha mambo kikatiba na kiusalama, miongoni mwa vipengele vingine, lakini akaonya kuwa mwanya wa kufikia hatua muhimu zaidi unazidi kuwa finyu.