Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Joto

Halijoto imevunja rekodi ya juu zaidi kote ulimwenguni mwaka huu wa 2023.
© Unsplash/Fabian Jones

“Ulimwengu unachemka, viongozi ongozeni”: Guterres

Kufuatia ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya hewa WMO kwa kushirikiana na lile la Kamisheni ya Muungano wa Ulaya ambayo imethibitisha kuwa mwezi huu wa Julai utavunja rekodi ya dunia ya kuwa na joto kali ulimwenguni kote, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema takwimu hizi mpya ni uthibitisho kuwa ubinadamu umeketi katika kiti cha moto na kwamba lazima hatua zichukuliwe haraka.

27 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Jacqueline Woiso, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania anafafanua ni malengo yapi ya Maendeleo Endelevu yaliyoipa Multichoice Tanzania Ushindi wa Tuzo ya UN Global Compact. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ripoti ya hali ya hewa, jaribio la kutaka kutwaa madaraka kijeshi nchini Niger na uhifadhi wa bioanuwai barani Afrika. Katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunakuletea maana ya neno “NDOFYA". 

Sauti
10'
Wafanyakazi wa ujenzi katika kituo cha kuzalisha umeme wa maji cha Trung Son Vietnam
World Bank/Mai Ky

Msongo utokanao na ongezeko la joto utasababisha hasara sawa na kazi milioni 80 ifikapo mwaka 2030-“ILO

Makadirio kwa kuzingatia ongezeko la joto la dunia la nyuzi joto 1.5 kufikia mwishoni mwa karne hii yanaonesha kuwa kufika mwaka 2030, asilimilia 2.2 ya jumla ya muda wa saa za kazi kote duniani itapotea kutokana na joto kali, na ni hasara sawa na nafasi za kazi milioni 80.  Maelezo zaidi na Patrick Newma

 

Sauti
2'31"