Uchaguzi wa disemba ni fursa ya kihistoria kwa DRC-UN
Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamehitimisha ziara yao ya saa 72 nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC na kuahidi kuunga mkono mchakato kuelekea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi disemba mwaka huu huku wakisihi uchaguzi huo ufanyike kwa uaminifu na amani.