Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

John Pombe Magufuli

UN Photo/Antonio Fiorente

UN yamenzi Rais John Magufuli kwa kupeperusha bendera nusu mlingoti

Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, bendera ya Umoja wa Mataifa inapepea kwa nusu mlingoti kuashiria maombolezo ya kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli aliyefariki dunia tarehe 17 mwezi huu wa Machi.

Rais Magufuli aliaga dunia jijini Dar es salaam naamezikwa leo nyumbani kwake huko Chato mkoani Geita nchini Tanzania.

Sauti
1'53"

18 MACHI 2021

Katika Jarida maalum la Umoja wa Mataifa hii leo, Grace Kaneiya anakuletea

-Salamu za rambirambi  zaendelea kutolewa kutoka Umoja wa Mataifa, mashirika yake na viongozi mbalimbali kufuatia kifo cha Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli kilichotokea jana Machi 17

- Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Profesa Kennedy Gastorn amesema Tanzania, Afrika na jumuiya ya kimataifa imepoteza kiongozi mwenye uthubutu na daima ataenziwa John Magufuli

-Wananchi wa Tanzania wamuomboleza Rais wao aliyeaga dunia jana Machi 17

Sauti
12'38"
UNHCR/Benjamin Loyseau

UNHCR yaomba radhi kwa Tanzania kutokana na sakata la nguo za msaada kwa wakimbizi zilizofanana na sare za kijeshi.

Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, Filipo Grandi akiwa ziarani nchini Tanzania  amesema Tanzania kwa muda mrefu imekuwa ni karimu hususan kwa wakimbizi ambao wanakimbia machafuko na rais wake John Magufuli amerejelea kuwa ukarimu huo hautafika mwisho.

Akizungumza na waaandishi wa habari pindi tu baada ya mazungumzo yao ya faragha na Rais John Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es salaam, Bwana Grandi amesema,

Sauti
2'17"

Guterres kuzungumza na Rais Magufuli wa Tanzania

Kufuatia mauaji ya walinda amani 14 wa Tanzania huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC siku ya Alhamisi na wengine zaidi ya 44 kujeruhiwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres muda wowote sasa atazungumza kwa njia ya simu na Rais John Magufuli wa Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nchini Tanzania, Balozi Augustine Mahiga amesema hayo akihojiwa na Idhaa hii kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam.

(Sauti ya Balozi Augustine Mahiga)