Chuja:

John kibego

UN Photo/Albert Gonzalez Farran

Kina mama wajasiriamali waneemeka na mafuta Uganda

Upatikanaji wa bidhaa ya mafuta nchini Uganda umeleta faraja kwa mamilioni ya wananchi ambao sasa wanaona nuru ya kupungua kwa bei ya bidhaa hiyo katika siku za usoni. Na neema hiyo sio kwa waendesha magari tu bali pia kwa wafanya biashara ndogondogo au wajasiriamali wakiwemo wanawake. Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego amewatembelea baadhi ya wanawake walioanza kunufaika na uwepo wa shughuli za uchimbaji mafuta katika eneo la ziwa Albert nchini humo ili  kupata ufafanuzi zaidi unagana naye

Choo chako ni salama?

Utafiti umebaini kwamba ukosefu wa vyoo safi  na salama ni hatarishi kwa afya ya binadamu. Takwimu za mashirika ya ufya ulimwenguni kama WHO na wengine zinaonyesha kuwa jamii zinazoishi katika mazingira yasiyo na vyoo salama zipo katika athari za kupatwa na milipuko ya magonjwa yatokanayo ya ukosefu wa matumizi salama ya vyoo kama kipindupindu na magonjwa mengine.

Dansi ya kitamaduni yaenziwa Uganda

Wakati shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO), linapigia chepuo utunzaji na ukuzaji wa utamaduni,  mjini Hoima nchini Uganda, waimbaji wa kitamaduni waliandaa tamasha la muziki kandoni mwa tamasha za muziki wa kisasa.

Je, lilishindana? Basi ungana na John Kibego katika makala ifuatayo...