Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani kwenye Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix amesema mahandaki yaliyochimbwa kuanzia Lebanon hadi Israel ni suala la wasiwasi mkubwa na ni ukiukaji wa azimio namba 1701 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Ikiwa mwezi huu ni umetimu mwaka mmoja tangu walinda amani 15 wa Tanzania wauawe huko Semuliki jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, Umoja wa Mataifa umesema katu hautosahau mchango wao na utaendelea kuenzi kazi yao.
Umoja wa Mataifa umetoa wito wa nchi wanachama kushikamana na kusaidia vita dhidi ya mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeida na ISIL kwenye ukanda wa sahel barani Afrika.
Amani ya kudumu na endelevu haitopatikana nchini Sudan Kusini endapo jamii hususan wanawake hawatoshirikishwa katika mchakato wa kuileta. Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa operesheni za ulinzi wa Umoja wa Mataifa Jean Pierre Lacroix baada ya kukutana na wanawake wakimbizi wa ndani kwenye eneo la Bentiu nchini humo.
Mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukianza leo, wakuu wa nchi na viongozi wa serikali wa nchi zinazochangia kwenye operesheni za ulinzi wa amani wanakutana kujadili jinsi ya kukabiliana na changamoto za ulinzi wa amani.
Licha ya kupunguzwa kwa bajeti na kuongezeka kwa majeruhi na vifo miongoni mwa walinda amani, bado ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa unabakia kuwa nyenzo muhimu katika kuchagiza amani na utulivu duniani, amesema mkuu wa operesheni za ulinzi wa aman iza Umoja wa Mataifa.
Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani kwenye Umoja wa Mataifa, Jean-Pierre Lacroix ametaka ushirikiano zaidi katika kukabiliana na changamoto zinazokabili shughuli za polisi wa chombo hicho, UNPOL, wanaohudumu kwenye operesheni za ulinzi wa amani.
Ziara hii ya pamoja ni utekelezaji wa mpango wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na mwenyekiti wa Kamisheni ya AU Moussa Faki Mahamat wa kutaka pande mbili hizo zishirikiane katika kufanikisha ajenda zao za amani na maendeleo.
Operesheni ya usaidizi wa ujenzi mpya nchini Haiti itafanikiwa tu endapo uhusiano kati ya serikali ya nchi hiyo na na operesheni mpya ya ujenzi ukiwa mzuri.