FAO yapokea ufadhili wa kuendeleza uhifadhi wa wanyamapori na usalama wa chakula
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limekaribisha mchango wa zaidi ya dola milioni 27 uliotolewa na Muungano wa Ulaya kwa ajili ya utekelezaji wa miradi endelevu ya wanyamapori ambayo inaimarisha uhifadhi wa bioanuwai barani Afrika.