Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Jamhuri ya Afrika ya Kati

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha sita kutoka Tanzania (TANBAT 6) wakiwafundisha mapishi wanakijiji cha Moro nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati.
TANBAT 6/Kapteni Inyoma

TANBAT6 watoa mafunzo ya mapishi na ujasiriamali kwa wanawake wanakijiji cha Moro, CAR

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 6 kutoka Tanzania (TANBAT 6) wanaohudumu chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya kati, CAR (MINUSCA) wametoa mafunzo ya upishi kwa vikindi vya wanawake wa Kijiji cha Moro kilichoko takribani kilometa 50 kutoka Mji wa Berberati, jimboni Mambere Kadei yalipo makao makuu ya kikosi hicho. 

Sauti
2'11"
TANBAT 6/Kapteni Mwijage Inyoma.

TANBAT 6, Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wapokea pongezi kutoka JWTZ na MINUSCA 

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa Kikosi cha 6 cha kutoka Tanzania TANBAT 06 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) wamepokea ugeni na salamu kutoka Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia ujumbe uliongozwa na Brigedia Jenerali George Mwita Itang’are aliyewakilisha salamu za Mkuu wa Majeshi ya Tanzania kutokana na sifa nzuri anazozipokea kutoka MINUSCA kuhusu kikosi hicho. Kutoka mjini Berbérati mkoani Mambéré-Kadéï, Afisa Habari wa TANBAT 06 Kapteni Mwijage Inyoma ameshiriki mapokezi ya ugeni huo, anaripoti.  

Sauti
3'42"
1.	Brigedia Jenerali George Mwita Itang’are akisalimiana na Afisa wa UNPOL baada ya kuwasili uwanja wa ndege Berbérati mkoani Mambéré-Kadéï nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR.
TANBAT 6/Kapteni Mwijage Inyoma

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wapokea pongezi kutoka JWTZ na MINUSCA

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa Kikosi cha 6 cha kutoka Tanzania TANBAT 06 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) wamepokea ugeni na salamu kutoka Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia ujumbe uliongozwa na Brigedia Jenerali George Mwita Itang’are aliyewakilisha salamu za Mkuu wa Majeshi ya Tanzania kutokana na sifa nzuri anazozipokea kutoka MINUSCA kuhusu kikosi hicho.

Sauti
3'42"
Walinda amani wanahamasisha jamii kufanya shughuli za maendeleo kwa ajili ya nchi yao ya Jamhuri ya Afrika ya Kati
© MINUSCA

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wametufundisha kutumia majembe – Wakulima CAR 

Wananchi wa Kijiji cha Difolo katika viunga vya mji wa Berberati mkoa wa Mambéré-Kadéï nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wamewashukuru walinda amani wa kikosi cha 6 kutoka Tanzania kinachohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo (MINUSCA) baada ya wanalinda amani hao kuwafundisha wananchi hao kulima kwa kutumia jembe la mkono badala ya kulima kwa kutumia panga.  

© MINUSCA

Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wametufundisha kutumia majembe – Wakulima CAR

Wananchi wa Kijiji cha Difolo katika viunga vya mji wa Berberati mkoa wa Mambéré-Kadéï nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wamewashukuru walinda amani wa kikosi cha 6 kutoka Tanzania kinachohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo (MINUSCA) baada ya wanalinda amani hao kuwafundisha wananchi hao kulima kwa kutumia jembe la mkono badala ya kulima kwa kutumia panga. Kapteni Mwijage Francis Inyoma ni Afisa Habari wa kikosi hicho ameandaa makala hii. 

Sauti
4'16"
Luteni Kanali Amin Stevin Mshana (katikati), Mkuu wa TANZBATT 6 akiwasili Berbérati, Mambéré-Kadéï, Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR.
TANZBATT 6/Kapteni Mwijage Inyoma

TANBAT 5 yakabidhi jukumu la ulinzi wa amani wa UN kwa TANBAT 6 nchini CAR

Kikosi cha 5 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANBAT 5 kilichokuwa kinahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA, kimekamilisha muda wake  na kukipisha kikosi kingine cha 6 nacho kutoka Tanzania, TANBAT 6 ambacho kitaendeleza jukumu hilo. Kutoka Berberat, Kapteni Mwijage Inyoma ni Afisa Habari wa TANBAT 6 ametuandalia taarifa hii. 

Sauti
2'35"
Meja Asia Hussein

TANZBATT 6 wakabidhiwa jukumu la ulinzi wa amani wa UN nchini CAR

Kikosi cha 5 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANZBATT 5 kilichokuwa kinahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA, kimekamilisha muda wake  na kukipisha kikosi kingine cha 6 nacho kutoka Tanzania, TANZBATT 6 ambacho kitaendeleza jukumu hilo. Kutoka Berberat, Captain Mwijage Inyoma ni Afisa Habari wa TANZBATT 06 ametuandalia taarifa hii. 

Sauti
2'35"