Mkuu wa MINUSCA kwa TANBAT6 - Zingatieni uhusiano mwema na raia
Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA, Jenerali Humphrey Nyone amewataka walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu nchini humo chini ya MINUSCA kuendelea na moyo wa uchapa kazi huku wakizingatia kuepuka unyanyasaji na unyonyaji wa kingono.