Hukumu ya kifo dhidi ya wauaji wa Khashoggi ni zahma juu ya zahma:Callamard
Mtaalam maalum wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji na mauaji ya kiholela Agnes Callamard amesema ameshtushwa sana na hukumu ya kifo waliyopewa wanaodaiwa kumuua mwandishi wa Habari wa Saudia Jamal Khashoggi huku walioamuru mauaji hayo wakiachwa bila kuguswa.