Vitisho vya matumizi ya nyuklia kwa makusudi au vinginevyo vinaongezeka hivi sasa na kuleta changamoto kama ilivyokuwa miaka 50 iliyopita wakati mkataba wa kudhibiti kuenea kwa silaha duniani, NPT ulipopitishwa.
Mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kudhibiti matumizi ya silaha, Izumi Nakamitsu amesema hayo leo mjini Geneva, Uswisi mwanzoni mwa kikao cha mapitio ya awali ya mkataba huo.
Amesema vitisho hivyo vitaendelea kuwepo iwapo mataifa yataendelea kuhifadhi silaha hizo akitolea mfano maeneo ya rasi ya Korea.