Skip to main content

Chuja:

Izumi Nakamitsu

Magofu ya mji wa Nagasaki, mita 800 kutoka kitovu cha shambulizi katikati ya mwezi Oktoba mwaka 1945
UN Photo/Shigeo Hayashi

Funzo kutoka kwa manusura wa Nagasaki lazima yauongoze ulimwengu kuondoa silaha zote za nyuklia-Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia maadhimisho ya miaka 75 tangu  bomu la atomiki lilipodondoshwa katika mji wa Nagasaki, Japan, amewasifu hibakusha, yaani waathirika wa shambulio hilo la bomu la nyuklia, ambao wamegeuza shida yao ya miongo kadhaa kuwa onyo juu ya hatari ya silaha za nyuklia na katika mfano wa ushindi wa roho ya mwanadamu.

UNICEF/Rich

Mbinu za kujipatia kipato ni muhimu kwa vijana ili kuepusha silaha ndogo

Mikakati mipya inahitajika ili kuweza kudhibiti kuenea kwa silaha ndogo na zile za kawaida ambazo kwa kiasi kikubwa ndio zinatumiwa kwenye migogoro duniani hivi sasa.

Mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa katika kudhibiti kuenea kwa silaha Izumi Nakamitsu amesema hayo leo jijini New York, Marekani wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati huu ambapo kuna mkutano wa tatu wa mapitio kuhusu udhibiti wa silaha ndogo na za kawaida.

Sauti
1'39"
UN Photo/Eskinder Debebe)

Hatua ya DPRK ni ya kuungwa mkono

Vitisho vya matumizi ya nyuklia kwa makusudi au vinginevyo vinaongezeka hivi sasa na kuleta changamoto kama ilivyokuwa miaka 50 iliyopita wakati mkataba wa kudhibiti kuenea kwa silaha duniani, NPT ulipopitishwa.

Mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kudhibiti matumizi ya silaha, Izumi Nakamitsu amesema hayo leo mjini Geneva, Uswisi mwanzoni mwa kikao cha mapitio ya awali ya mkataba huo.

Amesema vitisho hivyo vitaendelea kuwepo iwapo mataifa yataendelea kuhifadhi silaha hizo akitolea mfano maeneo ya rasi ya Korea.

Sauti
1'22"