Baada ya karibu wiki mbili za mapigano Kaskazini Magharibi mwa Syria mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yamekadiria kwamba takribani watu 180,000 wamelazimika kufungasha virako na kukimbia makazi yao , ikiwemo Watoto 80,000 na wote wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.