Baraza la Usalama lime laani shambulio lililo tokea huko Herat, Afghanistan
Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamelaani vikali mashambulizi ya kigaidi yanayoendelea nchini Afghanistan ambayo yanalenga raia likiwemo shambulio dhidi ya msikiti wa Guzargah huko Herat lililotokea jana tarehe 2 Septemba ambapo watu 18 waliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa.