Chuja:

IPCC

Mwanamke akiwa amembeba mwanaye wakati wa mafuriko mjini Jarkata Indonesia
© WMO/Kompas/Hendra A Setyawan

Mabadiliko ya tabianchi ni tishio kwa binadamu na afya ya dunia , hatua zahitajika sasa:IPCC Ripoti

Ripoti mpya ya jopo la kimataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi IPCC iliyotolewa leo imesema kuchukua hatua sasa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kunaweza Kuchukua hatua sasa “Kunaweza kulinda mustakabali wetu  kwani mabadiliko ya tabianchi yanayochochewa na shughuli za binadamu yanasababisha usumbufu wa hatari na ulioenea katika mazingira yetu na kuathiri maisha ya mabilioni ya watu kote ulimwenguni, licha ya juhudi zinazofanyika kupunguza hatari hiyo.”

Mtambo wa makaa ya mawe Tuzla, Bosnia
UNEP

Bila kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa kwa asilimia 7.6 lengo la nyuzi joto 1.5 halitafikiwa-Ripoti ya UNEP

Katika kuelekea mwaka ambao mataifa yataimarisha ahadi zao za ulindaji wa hali ya hewa zilizoafikiwa mjini Paris, ripoti mpya iliyotolewa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP, imeonya kuwa, ulimwengu utashindwa kufikia lengo la nyuzi joto 1.5 la mkataba wa Paris ikiwa dunia haitapunguza hewa chafuzi kwa asilimia 7.6 kila mwaka kati ya mwaka 2020 na 2030.

Katibu Mkuu wa UN António Guterres alipokuwa akizungumza hii leo tarehe 12 Desemba 2018 na wajumbe wanaoshiriki COP24 huko Katowice Poland
UNFCCC Secretariat/James Dowson

Guterres afananisha kutotimiza mkataba wa mabadiliko ya tabianchi na kujiua

Wakati ambapo majadiliano kuelekea mpango madhubuti wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi wa mwaka 2015 yakiendelea kukumbwa na vikwazo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo hii amerejea Katowice, Poland kuwapa changamoto zaidi ya viongozi 100 wa serikali ambao wanakutana katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabia nchi COP24 kufikia makubaliano na kuikamilisha kazi.