COP27 ikielekea ukingoni Guterres amewataka wajumbe kuzingatia hasara na uharibifu
Mkutano wa 27 wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi utafungwa angalau siku moja baadaye kuliko ilivyotarajiwa, ofisi ya Rais wa Misri imetangaza leo Ijumaa, ikitoa wito kwa wajadili kubadili msimamo ili makubaliano yaweze kufikiwa kuhusu mambo yaliyosalia yanayohitaji mshikamano.